Posts

Showing posts from May, 2017

Mambo Yanayokuzuia Kupata Furaha Ya Kweli Maishani Mwako

Image
Inaweza kuonekana ni kitu cha kawaida lakini kuwa na furaha ya kweli na ya kudumu ni kitu ambacho kinatafutwa sana na watu wengi. Ndio maana ukichunguza, harakati nyingi za kutafuta maisha zinalenga hasa kupata furaha. Hata hivyo pamoja na watu wengi kuitafuta furaha sana, lakini bado wengi pia wanaendelea kugubikwa na huzuni nikiwa na maana ni watu ambao wanaishi maisha hayana furaha sana kwa sehemu kubwa. Je, hebu tujiulize ni mambo gani ambayo yanasababisha mtu mmoja akawa na furaha au mwingine akaikosa furaha? Majibu ya maswali haya utayapata kwenye makala haya. Kikubwa fuatana nasi tuweze kujifunza pamoja. 1. Kufanya kazi usiyoipenda. Ipo asilima kubwa sana ya watu ambao wanafanya kazi ambazo mara nyingi wanakuwa hawazipendi sana. Kwa lugha rahisi wanakuwa ni watu wanafanya kazi ambazo hawazifurahii, kikubwa kwao inakuwa ni kutaka kuingiza kipato tu basi. Kama unafanya kazi ya namna hii ambayo huifurahii, lakini lengo lako ni kuingiza kipato basi elewa unabeba ...

Usilolifahamu kuhusu Tembo

Image
Bila shaka unamfahamu tembo aidha kwa kumuona kwa macho au kwa kumuona katika television. yawezekana ukawa hujui kwa undani jinsi tembo alivyo. Naomba nikuibie machache kuhusu mnyama huyu. Tembo, Pamoja na ukubwa wake, akitembea hana kishindo kabisa. Miguu yake kwa chini ni kama ina sponji hivi. Tembo ana uzito wa tani 7 Tembo jike hubeba mimba miaka miwili Tembo mtoto huzaliwa akiwa na kilo 80 Chakula cha tembo kwa siku ni kilo 300 na maji lita 40 Ni moja kati ya wanyama ambao hawapendi kelele. Wastani wa umri wake wa kuishi ni miaka 60. Tembo dume huwa na wanawake wawili mpaka wanne

Hatua 5 za kutatua tatizo lolote unalokutana nalo

Image
Hatua ya kwanza; jua kwa undani tatizo ni nini.  Najua utashangaa lakini ukweli ni kwamba wengi ambao wanakuwa na matatizo huwa hawajui tatizo hasa walilonalo ni nini. Na hivyo wanapokazana kulitatua wanashindwa, kwa sababu kama hujajua kiini cha tatizo huwezi kulitatua. Mara nyingi watu wamekuwa wakiangalia madhara ya tatizo, badala ya kuangalia chanzo kikuu cha tatizo. Huwezi kutibu tatizo kwa kutibu madhara, badala yake unahitaji kuzama ndani na kujua chanzo hasa cha tatizo ni nini. Na njia ya uhakika ya kufikia hilo ni kuuliza swali moja muhimu sana, KWA NINI. Uliza swali hili mara tano, yaani uliza kwa hatua tano. Kwa mfano kama tatizo lako ni kipato kidogo kwenye biashara yako, jiulize kwa nini kipato ni kidogo, jibu linaweza kuwa wateja ni wachache, jiulize tena kwa nini wateja ni wachache, hapo utapata majibu mengine, kwa kila jibu jiulize tena kwa nini? Mpaka utafika mahali na kuona hiki ndio kiini kikuu cha tatizo. Lijue tatizo vizuri, wahenga walisema kul...

NJIA SAHIHI ZA KUFANIKIWA KATIKA MAISHA.

Image
  Kuna wakati mwingine watu hushindwa kulitekeleza jambo fulani sio kwa sababu hawajui jambo hilo au eti kwa sababu hawana uzoefu wa jambo hilo, la hasha huo si kweli watu wengi wanashindwa katika kulifanya jambo fulani kwa sababu wanakosa"umakini" juu ya kulitenda jambo hilo. Na umakini ni ile hali ambayo ambayo mtu anakuwa nayo kutoka nafsini mwake katika kulitenda jambo fulani, lakini kulitenda jambo hilo bila kufikiri ni sawa na bure, hivyo kila wakati unahitaji kujenga umakini kwa kuwekeza nguvu na akili katika kufikiri na kutenda jambo hilo. Kamwe hutoweza kufanikiwa kama utaendelea ile tabia ya kutofanya vitu kwa umaikini. Kwani siri kubwa ya kushindwa kufanikiwa kwako ipo katika jambo hilo. Nasisitiza swala hili la kutenda mambo kwa umakini kwani pindi mtu anaamua kuwa makini humsaidia mtu huyo kuongeza ufanisi wa kiutendaji wa jambo husika na mara nyingine kutenda jambo kwa umakini huumfanya mtendaji wa jambo hilo kuepuka kurudia makosa katika kuli...

HULL CITY YAONDOLEWA RASMI LIGI KUU ENGLAND (EPL)

Image
Hull City yaondolewa kwenye EPL wakiwa na mechi moja ya kucheza kufuatia kipigo kikali walichopewa na Crystal Palace. Kikosi hicho cha Marco Silva kilipigwa na mshutuko na bao la dakika mbili na sekunde 11 baada ya kuanza kwa mechi. Mlinzi raia wa Italia Andrea Ranocchia alishindwa kuondoa mpira eneo la hatari hali iliyompta fusra Wilfried Zaha kutikiza wafu wa Hull City. Bao la pili la Christian Benteke lilitimiza mabao mawili ya Crstal Palace huku mabao mengine mawili yakifungwa na Luka Milivojevic, na Patrick van Aanholt. Sasa Hull watajiunga na Sunderland pamoja na Middlesbrough kusubiri msimu unaokuja. Hull City A.F.C. 18th in Premier League Premier League Today , 2:00 PM Selhurst Park Crystal Palace 4 - 0 FT Hull City Scores & schedule Mar 4  -  Premier League Leicester City 3  - 1 FT Hull City Mar 11  -  Premier League Hull Ci...

CONTE ASEMA HAYA BAADA YA UBINGWA EPL 2016/2017

Image
  Sunday, May 14, 2017   Msimu wake wa kwanza tu Uingereza ameipa Chelsea ubingwa wa nchini humo, huku likiwa kombe lake la nne ndani ya misimu minne mfululizo kama kocha. Baada ya kuipa Chelsea ubingwa huo Conte alizungumza na waandishi wa habari, moja kati ya vitu vikubwa kusema ni ugumu alioupata alipojiunga na ligi ya Uingereza na jinsi ilivyokuwa kazi kwao kubeba ubingwa. “Haikuwa rahisi kwangu kufanya hiki, kwani nilikuja hapa huku lugha inanisumbua na kukutana na wachezaji wengi wapya huku wakiwa wametoka kwenye msimamo ambao haukuwa mzuri” Conte anaendelea kusema kwamba ubingwa huo wa Chelsea msimu huu ni maalum kwa ajili ya wachezaji wake wote kwani anaamini walijitoa sana kwa ajili ya ubingwa huo. “Walionesha kuwa na hamu ya kutaka kufanya jambo kubwa sana na sasa naamini watakuwa nafuraha na msimu umetutendea haki, wakati tunaanza hatukuwa vizuri lakini sasa kikosi kimeimarika” alisema Conte. Conte anaamini mfumo wake wa 3-4-3 n...